

Lugha Nyingine
Argentinos marchan por memoria y justicia al cumplir 42 aos de último golpe de Estado Spanish.xinhuanet.com
Michezo ya 12 ya Dunia itafanyika mjini Chengdu, Mkoa wa Sichuan Kusini Magharibi mwa China kuanzia Agosti 7 hadi 17, 2025.
Julai 28, huduma ya usafiri wa treni za metro ya mji huo wa Chengdu, Chengdu Metro, ilizindua huduma ya kuwezesha kikamilifu malipo ya nauli kwa kutumia kadi za ng'ambo. Wasafiri wa kimataifa wanaweza sasa kutumia kadi mahsusi za benki za ng'ambo kugonga kuingia na kutoka kwenye milango ya metro, au kununua tiketi moja kwa moja. Laini zote za metro kwa sasa zimewekwa vifaa vya ukalimani kwa ajili ya kusaidia wazungumzaji wa lugha zisizo za Kichina.
Wakati wa michezo hiyo, Chengdu Metro itafuatilia kwa karibu mtiririko wa abiria na kuongeza uwezo wake wa usafirishaji, hasa katika maeneo ya kibiashara, vivutio vya utalii, na vituo muhimu vya kubadilisha laini za treni.
Chengdu Metro pia imeimarisha huduma yake ya wahudumu wa kujitolea. Vituo 70 vya wahudumu wa kujitolea vitawekwa kwenye maeneo ya michezo na stesheni kubwa za metro za karibu, vikitoa mwongozo na usaidizi ili kusaidia abiria wa China na wa kimataifa kuzunguka mjini kwa urahisi.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma